Breaking News
Loading...
Thursday, 9 April 2015

Info Post
Jamhuri Kiwello 'Julio' ana vituko kweli. Licha ya kupokea

kipigo cha mabao 8-0 kutoka kwa Yanga jana, Kocha huyo

mkuu wa Coastal Union amewaacha watu huo baada ya

kusema kuwa alitarajia kufungwa.
Julio ambaye yupo kwenye mkataba wa kuifundisha Coastal

Union kwa mkopo, amesema kuwa alitambua mapema kuwa

timu yake itafungwa na Yanga kutokana na kupewa taarifa

kwa kushtukizwa kuwa wanatakiwa waje Dar kucheza na

Yanga igawa wao hawakujiandaa na hilo.
"Nilitarajia kufungwa ingawa sio kwa idadi kubwa ya magoli

kama haya ya leo. Tulishtukizwa tukiwa kwenye bonanza

tukaambiwa tunatakiwa kucheza na Yanga. Sisi kwa kweli

hatukujiandaa kikamilifu kwa ajili ya mechi ya Yanga  ila

hatukuwa na jinsi ya kukataa kucheza," alilalama Julio.
Kipigo hiko kutoka kwa Yanga huenda kikamweka kikaangoni

Julio ambaye alipewa jukumu la kuinoa Coastal kwa muda

chini ya kocha James Nandwa ambaye muda mfupi baada ya

Julio kutua, alitimka nchini kwao Kenya akidai kutofurashwa

na ujio wake klabuni hapo.