Breaking News
Loading...
Thursday, 9 April 2015

Info Post
Kocha Mkuu wa Mbeya City Juma Mwambusi, amesema

kuwa atahakikisha timu yake inaibuka na ushindi kwenye mechi

tano za Ligi Kuu zilizobaki ili wamalize ligi wakiwa kwenye

nafasi nzuri.
Mbeya City inayoshika nafasi ya saba kwenye msimamo wa

ligi hiyo, ni miongoni mwa timu zilizo kwenye hatari ya kushuka

daraja kutokana na kuwa na tofauti ya pointi chache kati yao

na timu zilizo mkiani mwa ligi.
Akizungumza na Mwandishi wetu jana, Mwambusi alisema

kuwa mkakati wao kwa sasa ni kushinda mechi zao tano

zilizobakia ili kutimiza malengo waliyojiwekea mwanzoni mwa

msimu.
"Tuliweka malengo ya kumaliza ligi tukiwa kwenye nafasi nne

za juu kama tulivyofanya msimu uliopita. Mwanzoni

hatukuanza vizuri  ila kwa sasa naweza kusema kuwa tumerudi

kwenye mstari na tunataka kumaliza ligi vizuri," alisema

Mwambusi.
Mwambusi aliongeza kuwa licha ya timu yake kukumbwa na

jinamizi la majeruhi sambamba na beki wake Juma Nyosso

kufungiwa mechi nane, bado timu hiyo imeweza kusimama

imara na kuondoa hali ya kufanya vibaya mara kwa 

iliyowakuta mwanzoni mwa msimu.