Na Rob Hughes.
Imetafsiliwa na Kocha Somola
E-mail; Somolaa@yahoo.com
Facebook; Kocha Somola
LONDON-Raheem Sterling. Kwa usiku mmoja alikuwa ni kipenzi
cha kombe la Ulimwengu. Akitumiwa na
timu ya taifa ya Uingereza kama winga machachali, pale Manaus, Brazil,kuwa hangaisha
walinzi wa Italia kwa spidi yake kali na jinsi alivyofungua nafasi. Siku ile
aliwakumbusha wa Brazil mchezaji wao zamani, Garrincha, “Kandege Kadogo,”
ambaye alichezea timu ya taifa ya Brazil vizuri sana na kuchangamsha miaka 50
iliyopita.
Miezi
minne ilipita baada ya ile mechi ya kumbukumbuku aliyocheza Sterling ule usiku
pale Manaus, Sterling akapotea.
Akuchagaliwa katika wachezaji 11 wa taifa walioivaa Estonia mjini
Tallin. Kisa kikiwa alimwambia kocha wake anajisikia kuchoka.
Sterling
ana miaka 19.
Kukosekana kwake kwenye timu ya Taifa ya Uingereza, ambayo
ilikuwa inasaka kufuzu mashindano ya kombe la Ulaya kumezua mjadala mkali
kwenye mchezo, na si kwa Uingereza pekee, bali ulimwengu mzima. Kuna wengine wanamshangaa na kusema, kakijana
kadogo, kanacheza mala mbili, mala tatu kwa wiki katesemaje kamechoka?! Akajui
kwa mshahala mkubwa anaolipwa watu wengine wanaweza kufia uwanjani?!
Upande
mwingine wanamtetea kwamba, majukumu ni makubwa mno kwa mtoto mdogo anayecheza
mchezo wa watu wazima kwenye timu ya Liverpool na Taifa la Uingereza. Na ndiyo
inamfanya achoke, kiakili na mwili(burn out).
Lakini bado wengine wanamwagalia kwa jicho baya. Sana pale wanaposikia mameneja wa Liverpool
na timu ya taifa ya Uingereza wakilumbana, kipi muhimu, kuchezea club au
taifa? Liverpool inamtegemea sana Sterling,
tena zaidi baada ya kuwauuzia Barcelona, Luis Su’arez. Vile vile kumpoteza
Daniel Sturridge anaeuguza nyama ya paja, alilooumia akiitumikia timu ya taifa
ya Uingereza.
Liverpool
inauitaji sana, tena sasa hivi, ufundi na uwezo wake Sterling wa kuwafungua
walinzi wa timu pinzani. Ata mwishoni wa
mwaka jana, wakati Liverpool walipokuwa kwenye harakati ya kujaribu kutwaa
ubingwa wa ligi, baada ya miaka 20 kupita, ilikuwa ni Sterling zaidi, kulikoni
Su’arez na Sturridge, aliweyepaa matumaini ya kutwa ubingwa.
Liverpool
walimaliza washindi wa pili mwaka jana, na Su’arez aliondoka, na Sterling
alipewa kadi nyekundu, Miami-Marekani walipokuwa wakimenyana na Equador, mechi
ya kupasha kabla ya kombe la ulimwengu.
Na ata hivyo, Sterling alichaguliwa kuwa ndiye mchezaji wa kutegemewa wa
Uingereza, baaada ya ufundi aliyounyesha usiku ule pale Manaus, japo Uingereza
ilifungwa, alikuwa ni nyota siku ile.
Kuna
tetesi kwamba Real Madrid wanamtaka.
Na kwanini wasimtake?
Hatawafuraisha kama mchezaji wa zamani wa Uingereza aliyecheza winga, Laurie
Cunningham. Cunningham alikuwa nyota wa
Madrid na timu zingine alizochozea mpaka pale kifo cha ajali ya gari
kilipomkuta kule kule Spain.
Siku
zijazoo karibuni, Sterling ana majukumu makubwa mawili. Liverpool itakapomenyana na Queens Park
Rangers jumapili na jumatano ijayo watapokuwa wenyeji wa Real Madrid, katika
mechi ya kushindania kombe la washindi la Ulaya.
Q.P.R
ilikuwa ni timu ya kwanza kukiona kipaji cha Sterling. Aliiingia kwenye shule yao ya mpira(academy) akiwa na miaka 5, akitokea kwao
kwa asili, Jamaica. Alikuwa na kipaji
tangia mtoto, ata yeye, Sterling, anasema alianza kufanya jithada kuelekea kuwa
mchezaji wa kulipwa akiwa ana miaka 8 au 9.
Raheem
Shaquille Sterling anajielewa ana kipaji.
Anapoenda likizo Jamaica anatumia muda mwingi kuongea na rafiki yake,
Usain Bolt, jamaa mwenye kasi kali ulimwenguni.
Bolt anamwonea wivu Sterling,kwani anatamani ingewezekana wangebadilishana nafasi
ata kwa sekunde tu. Ingawa ndiyo Bolt
anafanya mazoezi na ile timu nyingine, Manchester United. Wivu wa Bolt si wa umaarufu bali upendo wa
mchezo kutoka moyoni.
Bolt
ana miaka 28, ndoto zake za kucheza mpira hazitatimia, sana sana ni kufanya
mazoezi na United.
Sterling
atakayetimiza miaka 20 Disemba, ndoto zake zote zinawezekana.
Ingawa kwenye michezo na maisha ni vigumu kutabiri kirahisi. Njia ya Sterling ilionekana nyeupe toka
alipoifungia Uingereza timu ya watoto wenye miaka chini ya miaka 17, kwenye
kombe la ulimwengu Mexico, miaka mitatu iliyopita. Sasa amezaa mtoto, msichana, aliyempata toka
kwenye uhusiano mfupi. Amewahi
kushitakiwa mala mbili kwa makosa ya kuwafanyia vurugu wanawake, lakini
akupatwa na hatia.
Liverpool
sasa wanamlinda sana jinsi anavyoishi, ndani na nje’ ya kiwanja. Na yeye ameamua kufanya mazoezi ya ziada ili
kujiongezea nguvu za kifua(kubeba vyuma).
Ingawa anasema ataki kifua kiwe kikubwa sana kwani labda bado
anakua. Anataka awe mwepesi, uwepesi utamsaidia
kukwepa walinzi wanaomkaba vibaya kwa nia ya kumuumiza.
Mjadala
wa kuchezea taifa au club siyo wa Sterling, wala si wa Liverpool, ila ni FIFA
na UEFA ratiba inayojaza mechi nyingi na kusababisha miili ya wachezaji kuchoka, kwani haiwapi muda wa
kupumzika wachezaji hao nyota.
Nyota
wengine kama Lionel Messi na Cristiano Ronaldo hawalalamiki kwa sababu mpira
ndiyo unawafanya wawe matajiri, lakini inawezekana wengi wakacheza kwa muda
mfupi kutokana na kuumia. Sterling
anaonyesha dalili za kuchukua nyazifa zao, ndoto ambazo zinaotwa na mamilioni
ya watoto.
Liverpool
na timu ya taifa ya Uingereza sasa wanajuzana data za wachezaji, wanatumia kwa pamoja
watalaamu wa mchezo na sayansi, kutunza rekodi na kupima kama mchezaji mwili
wake umechoka sana. Vile vile kwa
Sterling, hata waganga wa mawazo(Pychiatrist) wa Liverpool wanapokwenda kumwangalia
mazoezini, wapo tayari kuongea na mchezaji yoyote mwingine anayeitaji msaada
kwenye mazoezi ya timu ya taifa.
Wana historia
wanakumbusha, Raheem Sterling ndiye mchezaji mdogo wa pili kwenye historia
kuiwakilisha Liverpool, (baada ya Jack Robinson) ambaye alikuwa mchezaji wa
tatu mdogo kuiwakilisha Uingereza na wengine wachezaji wadogo kiungia timu ya
taifa miaka ya karibuni walikuwa ni Theo Walcott na Wayne Rooney.
Michael
Owen aliichezea timu ya Liverpool akiwa na miaka 17 na timu ya taifa lao miaka
18. Sasa hivi Owen ni mtoaji maoni
kwenye vipindi vya michezo na anakili kwamba, alifanya makosa kutohusikiliza
mwili wake kwa kucheza mechi nyingi akiwa mdogo.
Rooney, naodha wa timu ya taifa sasa, inaonyesha imeyapita
majaribu hayo, kwani karibu anafikisha mechi namba 100 na timu ya taifa.
Sterling
anawasikia watalaamu wakimwambia kuhusu kukua kwa mwili wake, lakini ni yeye
mwenyewe, ndiye anajua mwili wake unamwambia nini.
Habari hii iliandikiwa na Mwandishi Mashuhuli wa michezo,
Rob Hughes wa NYTimes.com na kutafsiliwa kwa ruhusa maalum kwa ajili ya
Mwaisabula Blog na Kocha Somola. Lengo
likiwa kufundisha na kuinua mpira wa Tanzania.
Ukitaka kuisoma kwa Kiingereza, “For Young Soccer Players, How Much Is
Too Much?” New York Times October 14, 2014. Naomba maoni yenu wadau, sana
sana kama nimekosea Lugha. Asante.