Breaking News
Loading...
Sunday, 28 September 2014

Info Post


            Hakuna anayeweza kupingana na mimi kwamba pesa ndio kila kitu, wengine wameshakuwa na misemo mingi sana wakiinadi pesa wakiitambuliha pesa utasikia wengine wakisema pesa ni sabuni ya roho sasa naamini wote ni wasafi na hata wachafu waajua nini maana na umuhimu wa sabuni katika maisha ya kila siku juu ya hili sina shaka kabisa na nina uhakika na imani zenu. Kila mtu anapogeuza shingo kutazama mashariki na magharibi, kaskazini na kusini huwa wanaangalia pesa na kuiwaza pesa katika akili zao. Hilo sio kwa watanzania tu bali kwa watu wote na duniani kote kwasababu hili ndilo suluhisho na njia kuu ya mawasiliano duniani. Huku kwetu tukiziita shilingi na wenzetu wanje wakiziita “dollar” au “paund”.
          Huwa nawakumbuka sana wana harakati wengi, wengine wakidai uhuru wengine wakidai Amani au mabadiliko katika nchi zao. Tusiende mbali sana hapa kwetu Tanzania alikuwepo mwana harakati mmoja ambaye alikuwa mwalimu wa mababu zetu na baadaye kuwa kiongozi wetu nadhani wote wanamfahamu Mwalimu Julius Nyerere na sitaki kuzungumza mengi kuhusu baba yetu wa taifa lakini naamini hakutumia pesa kama sabuni ya roho kushinda na kupata uhuru bali alitumia mikakati mikubwa sana na akili nyingi kupata hayo, hakuwa mwingi wa maneno bali mwingi sana wa matendo na hatua. Naamini na najua bila yeye na mikakati yake usingekuwa mahala tulivu penye kivuli ukipata kinywaji baridi na kuisoma hii makala.
             Sasa imefika watu wawaze maendeleo sana sana kuliko pesa. Ni kweli pesa ni sabuni ya roho lakini hutumika kuleta maendeleo au kubomoa kabisa maendelo katika jamii. Naamini juu ya hili tunayo mifano mingi sana kwani tunaona wenye pesa na walo na maendeleo na wenye pesa lakini hawana maendeleo sasa ni jukumu lako na uamuzi wako kuchagua upande unaokufaa wewe katika maisha yako.
              TFF, hiki ndicho chama kinachoshughulikia maswala yote ya mpira wa miguu ya hapa nchini kwetu Tanzania na kushika hisani ya chama kikubwa duniani cha FIFA katika taifa letu hili. Uongozi mzuri ni kitu nasaha na chenye mashiko makubwa sana katika muendelezo wa chama hichi ili kiweze kuyanyua mpira wa Tanzania ambao upo katiaka kiwango cha chini sana katika viwango vya FIFA. Mabadilko makubwa sana yanahitajika kwa ajili ya kunyanyua kiwango cha mpira kama ambavyo viongozi wa serikali yetu wanahangaika kuyanyua viwango vya elimu.
            Nafahamu wazi kuwa nchi yetu ina uchumi mdogo sana japo si masikini. Na pia naamini katika kila bajeti ya mwaka kuna fungu linatengwa kwa ajili michezo mbalimbali mmojawapo ukiwa ni mpira wa miguu ambao ndio una mashabiki wengi kuliko michezo mingine hapa nchini kwetu. Kwa hili nashawashika sana kuamini na kuona kwamba kila mwaka lipo fungu kwa ajli ya Tff. Na fungu hili si kingine bali ni pesa ambayo wengine wanaiita sabuni ya roho ambayo sijui ni kiasi gani lakini naamini inatosha kwa kiasi chake kusogeza hata hatua tatu au nne za mpira wetu hasa ligi yetu ya nyumbani yani Ligi kuu ya Vodacom.
             Najua unaweza kujiuliza maswali mengi ambayo hata mimi najiuliza kwamba hizi pesa kila mwaka huwa zinaenda wapi. Hilo mimi na wewe hatulifahamu lakini naamini pesa inatumika bila mikakati maalumu na hivyo kubakia kubeba jina la sabuni ya roho peke yake na siyo pesa kama chazo cha maendeleo. Hivi hawaoni jinsi ambavyo wenzetu  wanavyoambatanisha pesa na mikakati thabiti kabisa juu ya swala hili. Zipo nchi nyingi ambazo ni maskini kuliko sisi lakini wana maendeleo ya kisoka kuliko sisi, unafikiri kwanini, yote haya yanawezekana kama  viongozi wa Tff watapunguza mahojiano na kuamua kuthubutu kufanya mikakati na matendo ili kuboresha na kuweka misingi bora ya soka.
             Imefika wakati Jamali Malinzi na kamati yake yote waamue kutuonesha mambo mapya na mazuri, nataka na natamani katika uongozi huu mpya wa Tff ipo siku moja ntamchukua rafiki yangu Jerrylove au Allen wanipeleke nikashangae vipaji lukuki ambavyo vitakua vikiiandaliwa katika shule ndogo za mpira “Football Academy” au tutakwenda kushuhudia Simba au Yanga zikicheza mpira katika viwanja vyao wao wenyewe vya nyumbani na siyo uwanja wa taifa kama ilivyo Azam Fc pale Chamazi. Naamini mimi na wewe na hao rafiki zagu tutafurahi sana. Ni kweli pesa ni kila kitu lakini kama haina na haijawekewa mikakati endelevu basi pesa itabaki kuitwa sabuni ya roho na ni dhahiri itashindwa kabisa kuleta maendeleo na kunyanyua mpira. Naamini mwenyekiti wa Tff na viongozi wake wataitumia pesa kurudisha morali na muamko wa mpira na kuiweka ligi yetu katika hadhi ya kimataifa ili mimi na wewe shabiki mwenzangu tuweze kuingia katika historia ya moja ya watu kuwahi kushuhudia ligi bora na vipaji vya ajabu kama ilivyo kwa waajentina wanavyojivunia Messi na Maradonna.
                                                  Na,
                                                   Kelvin Kiimbila Jr,
                                                   0719580495,
                                                Kmichel350@gmail.com / Ngotejr@gmail.com.