Breaking News
Loading...
Sunday, 28 September 2014

Info Post

 
Wachezaji wa arsenal  Aaron Ramsey, Jack Wilshere na Mikel Arteta wataikosa mechi ya Galatasaray baada ya kocha arsenal wenger kuthibitisha watakua nje wiki ijayo- maana yake majeruhi hao wataukosa mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Galatasaray unaotarajiwa kuchezwa Jumatano
Pia wachezaji hao wapo kwenye hati hati ya  kuukosa mchezo wa Ligi Kuu ya England dhidi ya mahasimu wao wa jiji la londonChelsea Jumapili ijayo, wachezaji hao wote walipata majeraha jana katika sare ya 1-1 na Tottenham Hotspur Uwanja wa Emirates.
Wenger amesema: "Sifahamua muda mrefu kiasi watakuwa nje, lakini watakosekana wiki ijayo. Nafikiri Ramsey ni nyama (maumivu), na Arteta ni misuli ya nyuma ya mguu. Wilshere ni kifundo cha mguu,".