Wachezaji wa Taifa Stars wakiwa kwenye hoteli ya Tansoma Mnazi Mmoja wakisubiri usafiri wa awamu ya pili kuwapeleka mazoezini Gymkhana.
Akizungumza na MWAISABULA BLOGU mmoja
wa wachezaji wa Taifa Stars kwa sharti la kutoandikwa jina lake alisema kuwa
tangu walivyoanza mazoezi na timu hiyo ya taifa tatizo kubwa linalowasumbua ni kukosena
kwa usafiri wa uhakika kiasi kinachowapelekea kuchelewa kufika mazoezini.
“ usafiri umekuwa tatizo kubwa kwenye
timu ya taifa toka tumeanza mazoezi usafiri kwetu umekuwa changamoto kwetu
maana unatuchelewesha kwenye mazoezi
tumekuwa tukitumia gari dogo ‘Hiace’ ambayo uwezo wake ni mdogo kubeba wachezaji
wote, inabidi irudie mara mbili kitu ambacho kinafanya tuchelewa kuanza
mazoezi”. Alisema mchezaji huyo
Timu hiyo ambayo kwa sasa inafanya
mazoezi yake katika viwanja vya Gymkhana( Posta) kabla ya kusafiri mjini
Bujumbura Burundi kwa ajili ya mchezo wa kirafiki ulio kwenye kalenda ya
Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) September 7.
Kikosi kamili alichoteua kocha
Mholanzi, Mart Nooij kwa ajili ya mchezo huo ni makipa; Deogratias Munishi
(Yanga) na Mwadini Ali (Azam). Mabeki ni Said Morad (Azam), Oscar Joshua
(Yanga), Shomari Kapombe (Azam), Nadir Haroub (Yanga), Kelvin Yondani (Yanga SC),
Aggrey Morris (Azam), Joram Mgeveke (Simba) na Charles Edward (Yanga).
Viungo; Erasto Nyoni (Azam), Mwinyi Kazimoto (Al Markhiya, Qatar), Amri Kiemba (Simba), Himid Mao (Azam), Salum Abubakar (Azam), Said Ndemla (Simba), Said Juma (Yanga) na Haruna Chanongo (Simba).
Washambuliaji; John Bocco (Azam), Khamis Mcha (Azam), Simon Msuva (Yanga), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, DRC), Mbwana Samata (TP Mazembe, DRC), Mrisho Ngassa (Yanga), Mwegane Yeya (Mbeya City) na Juma Luizio (ZESCO, Zambia).
Viungo; Erasto Nyoni (Azam), Mwinyi Kazimoto (Al Markhiya, Qatar), Amri Kiemba (Simba), Himid Mao (Azam), Salum Abubakar (Azam), Said Ndemla (Simba), Said Juma (Yanga) na Haruna Chanongo (Simba).
Washambuliaji; John Bocco (Azam), Khamis Mcha (Azam), Simon Msuva (Yanga), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, DRC), Mbwana Samata (TP Mazembe, DRC), Mrisho Ngassa (Yanga), Mwegane Yeya (Mbeya City) na Juma Luizio (ZESCO, Zambia).
mazoezi yakiendelea kwenye viwanja vya Gymkhana asubuhi leo