Breaking News
Loading...
Sunday, 9 November 2014

Info Post




                               


Jana nilitabiri mechi 5,kati ya hizo ni mechi 3 tu ambazo zilichezwa.Na katika mechi hizo 3 nilipatia mechi 2 na kukosea mechi moja ya Mbeya city dhidi ya Stand united.Siku ya leo tutaangalia uchambuzi wa mechi mbili zilizobaki.
                                                            Simba Vs Ruvu Shooting
Timu ya simba ambayo haijashinda mechi moja mpaka sasa itaingia uwanja wa taifa kusaka ushindi wake wa kwanza dhidi ya Ruvu shooting.Ushindi wa simba leo utategemea zaidi viwango vya wachezaji wao wawili tegemezi Emmanuel Okwi na Jonas Mkude.Emmanuel Okwi ambae amehusika
katika kila goli ambalo simba wamefunga msimu huu anatarajiwa kuongoza safu ya ushambuliaji ya simba akishirikiana na Elius Maguri.Jonas Mkude ambaye kwa sasa ndie moyo wa simba,anatarajiwa kuunganisha vyema safu ya kiungo huku pia akisaidiana na mabeki wake kutoruhusu bao.Ruvu Shooting wataingia kwenye mechi hiyo wakiwa na kumbukumbu ya kupigwa bao 1 kwa bila na Coastal union ila kwa leo sioni kama timu hiyo itapata matokeo.
UTABIRI     Simba 3 Vs 1 Ruvu Shooting
                                                            JKT Ruvu Vs Ndanda Fc
Maafande wa Jkt Ruvu wataingia kwenye uwanja wa chamanzi wakiwa na hasira ya kupoteza mechi iliyopita dhidi ya Polisi morogoro kwenye uwanja wa chamanzi.Ndanda iliyoiadabisha Azam fc kwenye uwanja wa Nangwanda sijaona wataendelea kumtegemea nyota wake massawe kupata pointi 3 kwenye mechi ya leo itakayopigwa kwenye uwanja wa chamanzi.
UTABIRI JKT Ruvu 1 Vs Ndanda 0 Fc