Breaking News
Loading...
Monday, 10 November 2014

Info Post

Simba ilionekana kutawala kila idara katika mchezo huo.Tangu mwanzo mpaka mwisho wa mchezo Simba ilionekana kuwa na dhamira ya dhati kushinda mchezo huo.Shukrani za pekee zimuendee Okwi aliyekuwa mwiba mkali kwa mabeki wa timu ya Ruvu Shooting.Jonas Mkude na
Awadh Juma walicheza vyema kwenye nafasi  ya kiungo huku Rajab Isihaka na Nahodha Owino wakitengeneza ukuta mkali.

Kwa upande wa Ruvu Shooting walicheza vyema kipindi cha kwanza lakini kipindi cha pili waliingia na akili ya kutafuta sare kuliko ushindi jambo ambalo liliwagharimu.

Ushindi wa Simba Jana umewarudisha katika hali,kinachotakiwa ni kushinda mechi nyingi zaidi ili kuongeza kujiamini.