Kama unamini
kwenye bahati basi kasome maisha ya Vince Lombard.Hakuna mtu aliyetegemea kuwa
Lombard atakuwa mtu wa kukumbukwa kwenye ardhi ya Marekani.Lakini Lombardi
aliamini ipo siku juhudi zake zitamfikisha
kwenye ndoto zake.Ndivyo ilivyokua,Mpaka sasa Lombardi anahesabiwa kama
kocha bora kuwai kutokea kwenye ardhi ya marekani.Lombardi ni kocha mwenye
mafanikio zaidi kwenye ligi ya marekani. Japo watu wengi walikua wanamuhesabu
kama mtu mwenye bahati,Lakini Lombardi mpaka anafika alipofika alikua anaamini kwenye
kujituma.”Football is like life,It requires
Preseverance,Self-denial,Hardwork,Sacrifice,Dedication and Respect for
Authority”.(“Mpira ni kama maisha,Unahitaji uvumilivu,kujinyima,Kujitma,kujitoa
na kuheshimu mamlaka”).Hiyo ni kauli kuu ya bwana Lombardi katika
mchezo pendwa
wa mpira wa miguu. Kauli hiyo ilikuwa ikiwalenga haswa wachezaji wavivu.Bila
shaka kauli hiyo ina ukweli mtupu ndani yake. Ukiangalia wachezaji wote
waliofanikiwa Duniani lazima wawe na vitu alivyovisema Kocha Lombardi.
Nashukuru
Mungu kwa kuniwezesha kuangalia timu zote zinazoshiriki ligi kuu Tanzania bara
msimu huu.Wakati naendelea kuangalia ligi hiyo nilikua naendelea kutafuta
wachezaji walioelewa maneno ya hekima ya Lombardi.Mara nyingi nikawa mbaguzi
kwa kufuatilia zaidi wachezaji wetu(Watanzania) kuliko wachezaji wa
kigeni.Wachezaji wetu wengi wamepitwa
kabisa na busara za bwana Lombardi.Wachezaji wengi,waaliyadanganya macho yangu
kwa viwango vyao.Msuva ,Mkude na Ame Ally angalau waliupoza moyo wangu.
Nikaamua
kulitupa jicho langu pia kwa hawa wanaojiita ‘Maprofeshino’.Nikafikiri kuwa wao
watanionesha tofauti kidogo.Lakini nikagundua kuwa maprofeshino hao nao wengi ni waongo.Katika mechi chache hizi nilizoangalia sikuona haja ya
kuwa na wachezaji wa kigeni watano katika timu.Eti Jaja na kwizera nao ni
wachezaji wa kulipwa?,Hii ni hatari.Wachezaji hao hawana msaada kwenye timu zao
kuwazidi wachezaji wetu wa ndani.Siwezi kumchezesha jaja wakati kuna Tegete na
Javu kwenye benchi.Siwezi kumpa nafasi ya hata kukaa kwenye benchi la wachezaji
wa akiba mtu kama kwizera.Azam nae wanae ‘Profeshino’ Ismail Diarra ambaye
anakula pesa za mzee bakhresa bila kugusa uwanjani.
Labda
kama sielewi maana halisi ya kuwa na wachezaji wa kigeni hapa nchini.Lengo kuu
la watu hawa ni kuleta changamoto kwenye ligi yetu na kuwapa changamoto
wachezaji wetu.Lakini wengi wao hawana tofauti na wachezaji wetu wa
ndani.Matatizo ya wachezaji wengi ni yale yale aliyoyasema bwana
Lombardi,Kutokujituma,Kutojitoa,Kutokua na bidii,Kutokuwa wavumilivu na wengine
kufikia hatua hata ya kukosa heshima kwa watawala wao.Hakuna mengine zaidi ya
hayo.
Waswahili
wanasema kwenye msafara wa mamba hawakosi kenge.Licha ya wachezaji wengi wa
timu zetu kukosa mambo muhimu yanayowafanya wasifikie ubora wao,Lakini kuna
wachezaji ambao wamekua vioo vya wachezaji wavivu ligi Tanzania bara.Mpaka ligi
ilipofika nimemuona mchezaji mmoja tu ambaye ni mfano wa kuigwa kwa wachezaji
wetu na hata hawa ‘maprofeshino’.Si mwingine ni Emmanuel Okwi.Mguu wa Okwi
hausemi uwongo na wala akili yake haidanganyi hasilani.
Pamoja na
Simba kutofanya vizuri mpaka sasa lakini Okwi ameonyesha tofauti kubwa kati
yake na wachezaji wengine.Okwi ni mchezaji anayejituma
,anayejitoa,mvumilivu,mwenye bidii,anayejinyima na pia mwenye heshima kwa
mamlaka iliyo juu yake.Kuhusu kujituma na kujitoa kwake bila shaka kila mmoja
atakuwa shahidi,Anachofanya Okwi huwa nakifananisha zaidi na anachokifanya
Sanchez wa Arsenal.Popota mpira ulipo utamkuta okwi karibu yake.Pale simba
wanaposhambulia ujue mpira upo kwenye mguu wa Okwi.Pale Simba wanapofunga goli
ujue limefungwa au kutengenezwa na okwi.Hakuna goli la simba lilofungwa bila
mchango wa okwi,Kati ya magoli 7 simba ambayo wamefunga,Matatu yamefungwa na
okwi,matatu yametengenezwa na okwi pia moja limefungwa kwa mpira wa adhabu
baada ya okwi kuangushwa karibu na eneo la hatari la timu pinzani.Kila unapotaja
simba lazima utaje jina la Okwi,Kila unapozungumzia ligi kuu Tanzania utakua
mchoyo kama hutomzungumzia mwanaume huyu.Pia Okwi amekuwa mvumilivu sana,pamoja
na chokochoko zinazoendea klabuni,tena nyingine zikimhusu yeye dhidi ya
wachezaji wenzake.Lakini aliziba masikio na kufanya yale yaliyomleta Tanzania
ndani ya uwanja.
Tatizo
linakuja kwa wachezaji wetu wengi kuamini sana kwenye bahati kuliko juhudi.Tena
wengi wataacha kuiga mazuri na juhudi ya
Emmanuel Okwi badala yake watakaa chini kutafuta mbinu za kummaliza
Okwi.Wachezaji wengi wa Afrika wamejawa na mioyo ya husuda kwa watu haina ya Okwi.Lakini hiyo haitawasaidia
kitu.Wachezaji wetu pamoja na hawa maprofeshino upepo hawana budi kuwa na roho
ya kujituma kama aliyo nayo Okwi,Inabidi wabadilike na kuona mpira kama sehemu ya maisha yao,Kujituma na kuongeza
bidii kwao Uwanjani ndio kutawaletea manufaa kwenye maisha yao.Wasipofanya hivo
wakubali kuendelea kubuluzwa na profeshino wa ukweli Emmanuel Okwi,Kwani mpaka
sasa ni yeye pekee ndie amesikiliza na kuzifanyia kazi nasaaa za Vince
Lombardi.
Na
Allen Kaijage
0655106767