Breaking News
Loading...
Friday, 7 November 2014

Info Post



           Wiki tatu zilizopita moja wa magwiji wa soka Duniani Johan Cryuff alimualika Xavi Hernandez kufungua moja ya kiwanja cha soka kwa ajili ya vijana wa mtaanii.Kiwanja hiko kilichofunguliwa kwenye mtaa wa Terrassa nchini Spain kilipewa jina la Xavi.Xavi ambaye mitandao mingi Duniani inamtambua kama mchezaji bora wa muda wote katika nchi ya spain alikuzwa katika viwanja hivyo vya mtaani kabla hajachukuliwa na klabu ya Barcelona akiwa na umri wa miaka 11.Kwenye karne yetu hakuna mchezaji  fundi wa kupiga pasi kuliko Xavi.Umaridadi wote wa Xavi tumeuona kwasababu ya viwanja bora alivyocheza tangu  akiwa chipukizi mpaka hivi sasa.Usingeweza kuuona na wala huwezi kuuona kamwe Ubora na pasi maridadi za Xavi kama siku moja atacheza kwenye uwanja kama wa jamhuri.Bado nawaza  kama Xavi angezaliwa Tanzania?.Bila shaka tusingeweza kuona utamu wa miguu ya xavi hasilani kama tunavyoona akiwa kwenye uwanja wa camp nou.
          Wakati naangalia mechi ya Simba na Mtibwa nikamuwaza Xavi Hernandez,Nikafikiria kama angeweza kufanya kile alichoshindwa kufanya mkude ndani ya uwanja wa jamhuri.Nikagundua ningemuonea huruma Xavi kama  nilivokua nauonea huruma mguu wa mkude.Kila akijaribu kuonesha thamani ya mguu wake nyasi za uwanja wa jamhuri ziligeuka kuwa kizingiti kwake.Pasi ya mkude kabla ya kumfikia Ndemla lazima ipite kwenye mashimo matatu ya uwanja wa jamhuri.Kabla ya kumfikiria Shaban Nditi kuzuia mpira lazima kwanza ufikirie ni jinsi gani ya kukwepa mashimo hayo yaliyokithiri kwenye uwanja wa Jamhuri.Ubovu wa uwanja wa jamhuri haukuwa na athari kwa simba pekee bali hata kwa wenyeji Mtibwa Sugar.Si Simba wala Mtibwa iliyopiga pasi nyingi kuliko mashimo ya uwanja wa jamhuri.Kama ningekuwa natoa takwimu za umiliki wa mpira ningetoa 40% kwa mashimo na nyasi za uwanja wa jamhuri,32% kwa Simba na 28% kwa Mtibwa Sugar.
             Uwanja wa jamhuri si kiwanja kibovu pekee Tanzania bali ni mfano wa kiwanja kibovu Tanzania.Ukiondoa Uwanja wa Taifa na Chamanzi hakuna kiwanja kingine kinachotumiwa kwenye ligi kuu Tanzania chenye sehemu nzuri ya kuchezea mpira.Ntaanzaje kumhukumu  coutinho au Niyonzima kama anacheza kwenye uwanja mbovu kama wa kaitaba.Ntapataje ujasiri wa kuanza kuiita ligi yetu bora kama viwanja tulivyonavyo ni vile vile vya enzi za mwalimu.?
            Kwa hili ntailaumu Tff  pamoja na wamiliki wa viwanja hivyo. Tanzania ni sehemu pekee ambapo viwanja vya mpira wa miguu haviheshimiwi.Sijawai kusikia hata siku moja msanii kutoka  uingereza anafanyia  tamasha lake la muziki kwenye uwanja wa wembley au Old Traford.Lakini Tanzania uwanja huo huo wa kuchezea mpira pia kufanyia matamasha ya muziki.Tena mara nyingine utakuta leo kuna tamasha la muziki na kesho kuna mechi ya Mtibwa na Simba kwenye uwanja huo huo mmoja.Matamasha hayo yanachangia kwa kiasi kikubwa uharibifu wa viwanja vya soka, Hakika vitendo hivo ni kuukosea heshima mchezo wa soka.
            Kwa upande mwingine timu zinapocheza kunakuwa na mapato kwa ajili ya viwanja.Lakini mapato hayo huwa hayendi kwa ajili ya matengenezo ya viwanja husika zaidi ya kuishia kwenye matumbo ya wahusuda wachache.Wamiliki wa viwanja wanajali kujinufaisha tu na viwanja hivyo pasi na kujali ubora wa viwanja vinavyowaingizia mapato.
            Nikirudi kwa upande wa Tff ntawalaumu kwa kushindwa kuweka masharti ya vigezo vya viwango vya viwanja vinavyopaswa kutumiwa kwenye ligi kuu Tanzania.Tff ingekuwa na msimamo mkali kwa wamiliki wa viwanja tusingekuwa na viwanja vibovu Tanzania.Tatizo la shirikisho letu wamekubali kuwa bidhaa rahisi kwa kila kitu kinachohusu makubaliano.Viwanja vya Tanzania kwa asilimia kubwa vinamilikiwa  na chama cha mapinduzi.Kila siku huwa najiuliza kwanini chama hiko hakitaki kuachia viwanja hivyo kwenye mamlaka za soka ilihali wameshindwa  kuvikarabati na kuvisimamia viwanja hivyo.Nchi kama spain ilijenga viwanja vya soka ila ilipo ona majukumu yamezidi wakaamisha umiliki wa viwanja kwa timu husika za ligi kuu.
         Kama CCM haitakubali kurekebisha  Viwanja hivyo sambamba na kutoruhusu mambo mengine yasiyohusu soka kufanyika ndani ya viwanja vya soka,Pia  kama hawatakubali kubinafsisha viwanja kwa mamalaka za soka basi tutaendelea kushuhudia viwanja vyetu kupiga pasi nyingi kuliko mkali Xavi Hernandez.
                                                                          Na Allen Kaijage
                                                                              0655106767
                                                                       kaijagejr@gmail.com