Goli pekee alilofunga Emmanuel Okwi limeipa vinara wa Ligi Kuu ya Soka ya Tanzania Bara Simba SC pointi tatu muhimu kabisa kwenye mbio za kuwania Ubingwa wa VPL .
Kwa matokeo hayo Simba SC sasa wanafikisha Pointi 52 , sita zaidi ya Yanga SC ambao wamebaki na mchezo mmoja mkononi huku zikiwa zimebaki mechi 8 kwa Simba na 9 kwa Yanga.
Okwi anafunga goli lake la 17 katika ligi ya VPL , matano zaidi ya wale wanamfuatia kwenye orodha ya Ufungaji, John Bocco na Obrey Chirwa.
Na Simba wanapata ushindi dhidi ya Mtibwa pale Morogoro baada ya majiribio ya misimu mitatu.