Klabu ya Azam FC inazidi kusuka kikos chake kwa ajili ya msimu ujao wa 2018/2019 kwa kunasa saini ya kiungo Mzimbabwe, Tafadzwa Kutinyu kutoka Singida United.
Kutinyu alikuwa na msimu mzuri sana uliopita na mechi yake ya mwisho ndani ya Singida United ilikuwa jana kwenye fainali ya kombe la FA ambapo aliweka kambani lakini Singida walipoteza mechi.
Azam baada ya kumnasa kocha mkuu kutoka Singida United sasa wameibomoa tena kwa kumnasa kiungo huyo mshambuliaji