Mshambuliaji Shaaban Idd Chilunda amekamilisha uhamisho wa kutua klabu ya nchini Hispania CD Tenerife kutoka Azam FC.
Wawakilishi wake , ONRESA Football Agency wamethibitisha hivyo kupitia ukurasa wao rasmi wa Instagram huku ikionesha picha zake za kusaini mkataba wake.
Chilunda ambaye msimu uliopita alikuwa mfungaji bora wa Azam akiweka kambani magoli 10 tayari amesaini mkataba wa miaka miwili ambapo atabaki klabuni hapo mpaka mwaka 2020.