Ni alhamis ya leo ambayo Dunia macho na
msikio yake yanaelekezwa nchini Brazil ,katika michuano mikubwa kabisa maarufu
kama kombe la Dunia safari hii ikishirikisha mataifa 32 na Afrika tukiwakilishwa
na Mataifa matano ambayo ni Nigeria,Cameroon,Ivory Coast,Ghana na Algeria,basi
tunawaombea kila ra heri wawakilishi wetu angalau mwaka huu na si tujitoe
kimasomaso,basi turudi nyumbani tujulishane mambo yetu.
Kwa wale Binadamu waliokuwa na kulelewa au kupita katika Mkoa wa Tabora mji mashuhuri kwa jina la mashujaa wa
Unyanyembe watanielewa vizuri,Mkoa huo ni maarufu mno kwa zao la Embe kuna
maembe ya aina nyingi tu Mkoani pale lakini nayatazama ya aina mbili tu,kuna
Embe Dodo na Embe Bolibo,desturi na kawaida ya embe dodo ni chungu mno likiwa
bichi lakini ni tamu mno likiwa limeiva tofauti na Bolibo lenyewe likiiva
linakuwa tamu lakini si kama embe Dodo,uzuri wa Embe Bolibo likiwa bichi ni
tamu mno na kama utalikata kata vipande
na kuliunga na chumvi na pilipili kwa mbali mno basi linakuwa tamu mno,ndio
utamu wa embe huo.
Mbeya City leo ni kama Embe Bolibo
ambalo msimu huu limechukua nafasi ya tatu ikiwa nyuma Azam Fc wana lambalamba
na vijana wa Jangwani Yanga Afrikan na
Binslum ameingia kuchanganya Chumvi na pilipili ni utamu ulioje utaupata msimu
ujao, nasema karibu sana Binslum
nyumbani, Mbeya ni moja kati mikoa inayoitwa Big Four yaani yenye chakula cha
kutosha kulisha nchi nzima lakini kizuri
zaidi ikiwa imepakana na Nchi mbili kubwa yaani Malawi na Zambia ,Kampuni ya Binslum Tryes co kupitia bidhaa yao ya
betri za RB anasema namwaga milioni 360
mkataba mnono kabisa wa miaka miwili ni vipi soka lisipigwe Mbeya, na ni
vipi Binslum asitengeneze biashara yake kiulaini katika nyanda hizo ni akili
ndogo tu ambayo haiitaji uende Chuo Kikuu kujua kuwa Binslum ni mtu wa soka
lakini ni mzuri mno kwenye Biashara,mbali ya kuwamwagia mpunga mbeya ,Mkurugenzi wa Kampuni hiyo Binslum anasema
anamwaga udhamini wake na pale Stand ya Shinyanga na Ndanda ya Mtwara sehemu iliyopakana kwa karibu zaidi na
Msumbiji unataka nini tena ni balaa,wasukuma na wamakonde wanacheka ,na Binslum
sasa anafanya biashara yake Tanzania,Malawi,Zambia na Msumbiji safiiiii.
Mfadhili huyo anaonesha ni jinsi gani
anavyokerwa na maendeleo ya soka ndani ya nchi hii ninawakumbuka Ramesh Pater
Kaka alivyokuwa akijitoa kwa ufadhili wa
kuisaidia Tukuyu Star enzi hizo na akina Shafi Bora walivyokuwa wakiifadhili
Majimaji ya Songea na kuzifanya timu hizo kuleta upinzani mkubwa katika soka
letu hadi zote kuchukua ubingwa ndio leo anataka kufanya Binslum.
Binslum ambaye ni mzaliwa wa Tanga na
akiwa na asili ya Tanga ambaye watu na wadau wa soka muda mwingi walimzoea na
kumjua kuwa ni mfadhili wa Coastal Union
na shabiki wa kutupwa wa Liverpool lakini ghafla ameustua Ulimwengu na
kuwaonesha yeye si tu mshabiki wa Tanga bali ni mpenzi halisi wa soka na kwamba
soka lipo ndani ya damu yake hasa, na sasa anaelekeza nguvu zake sehemu tofauti
na hadi nje ya mipaka ,nasema saafi saana Binslum.
Kampuni hiyo inayojihusisha na kuuza
Matairi na Mabetri ya gari imeonesha changamoto kubwa kwa kampuni zingine kujitokeza na kuzifadhili
timu nyingine na hasa ndogondogo.
Ili soka angalau lipige hatua tatu mbele inabidi tuwapate angalau
akina Binsulum kumi hivi ,ili ligi iwe na mvuto zaidi na zile timu ambazo
zenyewe zilijiwekea nadhiri kuwa ubingwa ni wao miaka yote basi zishike adabu,
kwa mtazamo tu wangu binafsi wachezaji wa Tanzania wote wana uwezo unaofanana
tofauti yao kubwa inakuja kwenye nguvu ya kiuchumi,zipo timu zinaingia katika
ligi ya Vodacom hazina uhakika wa kula, kulala na hata kupata posho za
siku,wachezaji wake wanacheza katika mazingira magumu mno kiasi cha
kushawishiwa wakati mwingine kucheza chini ya kiwango iwe kwa bahati mbaya au
kwa makusudi.
Lakini zipo timu chache mnoo zinacheza
zikiwa na uhakika wa kula,kulala,posho na usafiri ni vipi wachezaji wake wasiwe
katika kiwango kizuri muda mwingi kama sio muda wote ndio maana nasema soka
letu linaitaji watu wazalendo kama akina Binslum.