Breaking News
Loading...
Saturday, 2 August 2014

Info Post



Ni mwezi ambao  tayari tupo ndani ya mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani na Dunia yote macho na masikio yameelekezwa katika bara la Amerika ya Kusini katika nchi ya Brazil ambako kuna fainal za kombe la  dunia la mpira wa miguu maana ya soka,ni balaa watu wanakesha usiku kucha wakipigwa na mmbu kisaa tu ni soka.

Soka au mpira wa miguu ni mchezo wa ajabu mno,ni mchezo ambao unaweza kuleta furaha wakati wote na unaweza ukaleta maafa wakati wowote,kwangu mimi naona ni mchezo katili na wenye roho mbaya muda wote,kwa watu ambao ni vichaa kabisa wa soka ni nadra mno machozi kutokupatikana uwanjani,ndugu yangu Maico Richard Wambura ataungana na mimi kuwa soka ni mchezo katili.

Bahati mbaya nimezaliwa na kujikuta natumbukia katika ukichaa wa soka,watu wengi wananijua na kunifahamu kupitia iwe wakati nacheza,nikiwa kocha,nikiwa mchambuzi au nikiwa naandika makala,nimejikuta niko chizi tu wa soka.

Mchezo wa soka ni kama Dini tofauti na dini ni kwamba soka kila mtu analiangalia na kulisema anavyojua,Rais wa Fifa Sett Blarte anasema utamu ni kuzungumzwa mchezo unachezwa dakika 90 lakini unazungumzwa wakati wote,matukio yeyote ya ajabu kama Luis Suarez kumg'ata mtu jino  Cristiano Ronaldo kuaga mashindano kwa goli moja ,bao la Robin Van Persie lilivyokuwa tamu watu hawaelewi lilitokana na krosi au majaro soka lazima lizungumzwe ndo utamu wake hapo.

Rais wa TFF aliyemaliza muda wake Leodgar Shilla mwaka jana wakati akiongea katika tunzo la  Mwanaspoti la kuchagua wachezaji bora alizungumzia soka,kitu anachokikumbuka mpaka leo ni jasho lake na harufu ya viatu yeye na wenzake ndani ya chumba cha kubadilishia nguo wakati wa mapumziko,ilikuwa ni shashu ya ushindi ndo utamu wa soka huo

Ronaldo de Lima mmoja kati wafungaji bora waliopata kutokea katika Dunia hii,akikumbuka soka anasema kitu pekee alichokikosa katika soka kwa sasa ni kushangiliwa na watu wengi kwa mara moja leo pamoja na utajiri wake lakini hicho amekikosa kimo ndani soka.

Soka ni mchezo na juzi baada ya mchezo kati ya Ivory Coast kocha wao kijana mdogo kabisa Mfaransa Sabri Lamouchi alisema kwa masikitiko baada ya mechi kwisha kuwa ulikuwa ni mchezo wa kikatili mno na kwamba ni kweli Ugiriki walistahili kushinda lakini tungepata faida kama mechi ingemalizika katika muda wake.Ni maneno ya huzuni kwa upande ulioshindwa yakisemwa kwa huzuni kubwa mno lakini ni furaha kwa upande mwingine ndio maana tunasema soka ni mchezo katili.

Katika hali ya kawaida kabisa Nchi nzima ya Ivory Coast na waafrika kwa ujumla walikuwa wamebaki na dakika moja tu kukamilisha furaha yao mtu mmoja tu Georgios Samaras anaukwamisha mpira kimiani kwa njia ya penalt inayotolewa na Mwamuzi katika muda mbaya na katika mazingira hatarishi na hasa  kwa viwanja vyetu vya uswahili,na katika tukio jepesi mnooo,soka ni mchezo katili na mwamuzi anafanya ukatili wa hali ya juu mno kwa bara zima la Afrika.

Ivory Coast mashindano na wakongwe wake walioshiriki fainal hizi kwa mara ya tatu ndoto zao za angalau kufika robo fainal zikiyeyuka dakika moja ya mwisho kweli soka katili,nani alitegemea kizazi hiki kinachoondoka cha kina Didier Drogba,Yaya Toure,Solomon Kalou,Gervinho,Kolo Toure kiishie hapo kilipoishia hakuna soka ndio limeamua hatuna ujanja.

Mexico walijikuta kwenye hali mbaya juzi mbele ya Uholanzi kama ilivyowakuta Ivory Coast hadi tatu kabla ya mpira kwisha kwa muda wa kawaida na si wanyongeza walijikuta furaha yao ikiota mbawa kwa kujapwa magoli mawili ya haraka haraka ikiwepo na penalt ya utata kweli soka ni mchezo katili.

Wanaoongoza soka ni lazima wajue kuwa soka ni mchezo hatari,soka ni mchezo unaopendwa mno na kuna watu wamezaliwa katika soka,wamekulia katika soka,wapo ndani ya soka na maisha yao yote yanategemea sokaaa,ni lazima wautendee haki mchezo wenyewe,ni lazima wawe waadilifu,wakweli na wanyenyekevu kwa wanaopenda soka yaani kuanzia mashabiki,makocha,waamuzi,madactari wa michezo,waandishi wa habari za michezo na wahusika wote.

Wanaongoza soka wakiutendea haki mchezo wenyewe,wakatoa haki kila kuanzia kwa makocha kuwaelimisha kwa haki bila ubaguzi,kutoa gredi za kwa waamuzi anayestahili,waamuzi kuwa Fair ndani ya uwanja na mashabiki kuwa mashabiki si uhasma huenda soka likabadilika sio katili mno kama ilivyo sasa,ambapo soka limekuwa katili mno mtu mmoja anahatarisha maisha ya wengi mno mfano kwa kutoa penalt dakika za mwisho na ikiwa haina kichwa wala miguu,soka ni mchezo hatari na mchezo katili mnooo