Breaking News
Loading...
Monday, 4 August 2014

Info Post



Tayari jana ndio tumefikia tamati ya michuano yetu ambayo kwa kweli kuanzia TFF na sisi wadau tulikuwa na shauku kubwa ya kuhakikisha tunafuzu na kuingia ligi ya makundi kuumana na Zambia,Carpe Verde na Niger na baadaye tuelekee Morocco mwakani na wale vijana waelekee Benin lakini ndo tumekwama baad ya kuondolewa jana na Msumbiji kwa magoli 2-1 na vijana wetu juzi kufungwa na Afrika ya kusini 4-0. Sasa macho na masikio yetu turudi nyumbani tutengeneze mpira

TFF kupitia msemaji wake Boniface Wambura imetutangazia kuwa ratiba ya ligi itatoka mwezi mmoja kabla yaani Agost 20 tayari itakuwa uwanjani na kila timu itajua inaanza wapi na nani ili ijipange vizuri safi sana kwa hilo,Uongozi uliopita uliokuwa chini ya Leodgar Shilla Tenga ulifanya mambo mengi mazuri ambayo kimsingi ni lazima yaigwe na kuenziwa,iliweka utawala safi wa kujua nani anawajibika kwa hili na nani anawajibika kwa lile,ilikuwa sio rahisi Tenga kumshika ubaya kwa kuwa mambo yote aliyaacha kwa watendaji wake,wakati mwingine ni safi ingawa wakati mwingine ni tatizo.

Katika jambo ambalo mwandishi wa makala hii alikuwa akilipigia kelele kila kukicha ni mfumo wa ligi,jambo ambalo lilimweka mbali mno na utawala uliopita na kumuona msaliti na kutompa nafasi yeyote ya kusogea pale alipo katika taaluma yake na kuwaacha wadogo zake wakipaa kila kukicha.

Katika mengi mazuri waliyoyafanya moja la mfumo wa ligi kwangu mimi ilikuwa ni tatizo na naamini ndio limetufikisha hapa tulipo,Mkurugenzi wa Ufundi wakati ule jambo la kwanza kabisa akaua ligi zote za chini na kuanzisha ligi moja tu ya TFF ufa wa kwanza mbaya ambao sikuukubali hadi leo ,Tenga kwa kuwaamini mno watendaji wake akaubariki,mwaka 2007 ikachezwa ligi ndogo ya kubadili mfumo ili tuwaige watawala wetu waliotutawala yaani Waingereza kuanza ligi mwezi wa nane na kumaliza watano safi sana wote tulipongeza tukasubiri utekelezaji,hapo ndio ilikuwa ni kichekesho wenye kuona kwa jicho tukapiga kelele,wanaume wale walifumba macho na masikio yao hadi wanaondoka madarakani waliacha ligi ya miezi sita inachezwa na miezi sita wachezaji wamelala majumbani kwao na mishahara wakilipwa.

Ligi imekuwa ikianza mwezi agost mwishoni na mwezi wa novembar mosi inasimama hadi mwezi march au February mwishoni na ikifika April ligi imekwisha ukiangalia hapo mchezaji anakuwa uwanjani kwa muda wa miezi isiyozidi sita halafu tunajidanganya kuwa tunaiga mfumo wa Uingereza ambao wenyewe wakianza ligi Agost hawasimami hata iwe x mass hadi mwezi wa tano tarehe 15 na wakiwa wamecheza mechi za ligi 38  achilia makombe mengi yapo katikati hapo,ndio maana katika hilo nilipiga mno kelele na adhabu yake niliipata lakini bora iwe hivyo kwa maslai ya Taifa.

Uongozi mpya ulioingia madarakani chini ya Jamal Emil Malinzi ulipoingia madarakani uliunda kamati zake nyingi mnoo,mojawapo ya kamati iliyonivutia ni ile ya kutengeneza mfumo wa ligi na ikiongozwa na Profesa Mshindo Msola,haraka mno nilipiga hodi ofisini  Msola nikimuonesha kukerwa kwangu na mfumo uliopita na nilikuwa na kitabu changu cha zamani kidogo nilimuonesha mfumo wa ligi na ratiba za ligi kuanzia ligi daraja la pili hadi ligi ya Muungano za mwaka 1986-1990  jinsi wachezaji wetu walivyokuwa wakicheza mechi nyingi na muda mrefu jambo ambalo wachezaji wetu  leo wamelikosa,ndio maana nasema naisubiri kwa hamu ratiba hiyo kama itakuwa kama ile iliyopita basi soka litazidi kwenda kuzimuu.

FIFA wanasema ili mchezaji afikie kiwango cha kimataifa yaani cha ushindani ni lazima acheze mechi zisizopungua 40 kwa msimu mmoja sasa ni lazima tukae tujiulize wachezaji wetu wanacheza mechi ngapi,kama atacheza mechi zote za ligi kwa muda wa miezi hiyo sita atacheza mechi 26 tu ,na kama yupo timu ya Taifa ataenda akiwa hajafikia malengo ya soka lenyewe pungufu mechi 14 atakuwa ni kichekesho tu
Nilimwonesha Kaka yangu Mshindo Msola ligi ya miaka ikichezwa kwa muda miezi tisa bila kusimama,na kama timu ya Taifa ina michuano ligi yetu inaendelea kasoro ile timu itakayokuwa na wachezaji zaidi ya watatu,ratiba inaonesha ikiisha ligi yetu inakuja ligi ya Muungano,halafu Taifa  Cup yaani michuano ya mikoa ambayo haiwazuii wachezaji wa ligi kuu kucheza na mwisho timu bingwa inakwenda katika mashindano ya klabu bingwa ya vilabu katika ukanda wetu wa Afrika Mashariki na ya Kati.

Nilimdhibitishia Msola itakapofika suala la kujadili mfumo kama unadhani mawazo yangu ni sahihi niite kwenye kamati kimyakimya na siitaja posho yeyote nije nitoe mawazo yangu tunahitaji ligi bora na si bora ligi.

Inasikitisha leo Haruna Nyonzima ,Emanuel Okwi,Owino,Musoti,Kiiza na wengineo wa nje wanakaa muda mrefu katika nchi zao tofauti na sisi kwa Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu ambao ni nadra mno kuwaona nyumbani maana Samata me ni jirani yangu simuoni kabisa nyumbani.

Timu zinaingia mikataba mikubwa na minono kwa wachezaji wao lakini matumizi yao ni kipindi kifupi mno,haingii akilini uwe na kampuni na umwajiri mfanyakazi wako afanye kazi miezi sita na sita kalala kwa mkewe au mumewe halafu umlipe mshahara wa mwaka mzima utegemee kupata faida haiwezekani,ndio maana leo nasema yapo mazuri mengi mno aliyoyafanya Tenga ambayo Malinzi inabidi ayaendeleze lakini kwangu mimi hili kama TFF hii italiendeleza me natoa Shilingi yangu.