Breaking News
Loading...
Saturday, 27 September 2014

Info Post

                              
                  “Uaminifu unajengwa na ‘consistency’(msimamo)”  hayo ni maneno ya mwanasiasa nguli wa marekani ambaye ni Gavana wa 74 wa visiwa vya rhodes bwana Lincoln Chafee.Usemi wa bwana chamfee unanifanya niwakumbuke wachezaji waliokosa kitu kinachoitwa ‘consistency’.Wachezaji hao wengi  vipaji sana ila hawavumi  kwa muda mrefu.
                 Desemba 2007 wakati wa mechi ya Almeria na Barcelona washabiki wa Barcelona walidiriki kumzomea Ronaldinho Gaucho.Kuna baadhi ya watu walishangaa,Huku wengine wakijiuliza washabiki hao wametoa wapi ujasiri wa kumzomea Ronaldinho Gaucho.Ronaldinho ambaye amewapa makombe ya ligi mawili,na kombe la klabu bingwa ulaya moja,Tena akiwa kwenye kiwango cha hali ya juu.Bado wengi walijiuliza Hawa washabiki wa Barcelona wanawaza nini mpaka kumzomea mchezaji bora wa Dunia mara mbili mfululizo kwa miaka miwili iliyopita.Jibu ni kuwa Ronaldinho alikosa ‘consistency’.Kwenye umri wa miaka 27 aliokua nao bado alikuwa na uwezo wa kuwapa vitu zaidi mashabiki wa Barcelona.Ila hali haikua hivyo kama mashabiki walivyotarajia.Wazungu wanasema “too much expectation result to greater disappointment”.Mashabiki wa Barcelona bado walikua na matarajio makubwa kwa Ronaldinho lakini akawakatisha  tama kwa kiwango chake wasichokitarajia.Kadiri siku zilivyoenda kiwango cha Ronaldinho kilishuka jambo lililopelekea kufungashiwa virago vyake,na huo ukawa mwisho wa Ronaldinho ndani ya uzi wa Barcelona.
               Mchekeshaji maarufu Duniani raia wa mexico  Louis Ck aliwai sema “Kama ukifanya kazi kwa bidii na kutumia muda na nguvu nyingi kwenye kitu unachokifanya na kwa mwendelezo wenye msimamo(‘consistency’) lazima utapata matokeo mazuri kwenye hicho unachokifanya”.Nikiangalia wachezaji wengi wanaocheza soka la bongo hasa wale wanaopata majina kidogo wanakua na tabia kama za Ronaldinho.Wengi hawataki kufuata kauli ya Louis Ck.Wengi wamekosa vitu hivyo viwili yaani bidii na ‘consistency’.Kila nikimuangalia Uhuru seleman lazima nimkumbuke Ck.Uhuru seleman amekosa ‘consistency’ jambo linalohatarisha maisha yake ya soka.Wana Simba na Watanzania wengi walikua na matarajio makubwa kutoka kwenye miguu iliyobarikiwa ya Uhuru seleman.Ni mmoja wa wachezaji wenye vipaji maridhawa Tanzania lakini kiwango chake kimekua kikiporomoka kila unapomuona.Wakati naangalia mechi ya Coastal union na Simba niliona kiwango chake kibovu kabisa tangu nianze kumshuhudia.Bila shaka Uhuru seleman hafanyi mazoezi kwa bidii,Siku si nyingi mashabiki wa Simba watamkataa uhuru kwa kuanza kumzomea.Uhuru akiendelea hivyo maisha yake ndani ya Simba yatakua mafupi mno kama ya Ronaldinho ndani ya Barcelona.
                Upande wa pili wa shilingi wana habari mpya inayoitwa Jaja.Ukipita kwenye meza za magazeti bila kulikuta jina la jaja basi ujue ilo gazeti limepitwa na wakati.Kwa sasa jaja ni kipenzi cha mashabiki wa Yanga.Jaja anapendwa kwasababu amewapa mashabiki wa Yanga walichokihitaji kwa muda stahiki.Washabiki wa Yanga wengi walikua wana kidonda cha kuondoka kwa Emmanuel Okwi.Tena mbaya zaidi kwenda kwa mahasimu wao wakubwa.Mashabiki wa Yanga walihitaji mtu atakayewaaminisha kuwa Okwi si lolote kwao.Walikua wanahitaji faraja kuliko kitu chochote kwa muda huo.Na jaja hakufanya makosa akawafariji.Akawapa raha zilizowafanya wamsahau Emmanuel Okwi kwa muda.Mabao mawili  aliyoyafunga dhidi ya Azam yalikua dawa kwa ugonjwa uliokua ukiwasumbua  mashabiki wa yanga kwa wakati huo.
                Ila bado nawaza,Je jaja anaweza kuendeleza kiwango alichokionesha kwenye mechi ya Azam?.Hapa ndipo nnapomkumbuka Said Bahanuzi.Baada ya Yanga kufungwa goli 5 na Simba aliwapa mashabiki bao 6 kwenye kombe la Kagame,Mabao yake yaliiwezesha yanga kuchukua kombe la kagame na kusahau kipigo cha bao 5 walichokipokea miezi miwili kabla.Bahanuzi alijaa kwenye mioyo ya washabiki wa Yanga,Mpaka wakafikia kumuita habari ya mjini na wengine wakamuita Spider Man.Lakini leo hii hakuna mshabiki wa yanga anayemuelewa Bahanuzi,kwasababu ya kukosa ‘consistency’.
             Jaja najua hujui Kiswahili,Ila nna imani Ngasa,Kaseja na Yondani watakupa tafsiri ya hili muhimu nnalotaka kukwambia. Jaja inabidi ujue nini  wayanga wanataka kwa muda huu. Wanayanga wanataka kombe la ligi kuu ya Vodacom .Ili yanga wapate kombe la ligi kuu ya Vodacom wanahitaji mabao ya kutosha kutoka kwako.Jaja inabidi uwe na kiwango kisichopanda na kushuka yaani  uwe na‘consistency’ Ukiwa na kiwango kisichobadilika utafunga magoli na kuwapa yanga ubingwa.Hapo utakua umeshinda mioyo ya wanajangwani.Wana Yanga hawatakuelewa kwa sababu ulifunga magoli mawili dhidi ya azam ila watakuelewa kama utaendelea kufanya ulichokifanya dhidi ya azam.
             Lakini Jaja kwa ulichoanza kukionyesha kwenye Uwanja wa Jamhuri  unaanza kunipa mashaka,bado najiuliza  kama kweli yale magoli yako uliyofunga dhidi ya azam ndio kiwango chako halisi au uliamka vizuri tu siku hiyo.Bwana Jaja naomba ufanye hili kwa usalama wako.Mwenzako Said Bahanuzi asingekua Mtanzani angeshatupiwa virago vyake zamani sana.Naye Alikuwa Habari ya Mjini kama wewe.Usipokua makini na wewe utakuwa  habari ya mjini kwa miezi miwili kama alivyokua  Bahanuzi.Usipowapa wana yanga wanachohitaji watakuzomea,hawatokupenda tena na matokeo yake utaenda uwanja wa ndege kuelekea kwenu brazil bila kusindikizwa na vuvuzela  za yanga bomba.
                                                             Na allen kaijage
                                                               0655106767
                                                         kaijagejr@gmail.com