Breaking News
Loading...
Saturday, 6 September 2014

Info Post



                             Dennis Odhiambo (kulia) akichuana na Simon Msuva

 Nahodha wa klabu ya Thika United ya Kenya, Deniss Odhiambo ameiambia MWAISABULA BLOG kuwa amevutiwa sana na klabu ya Yanga na yupo tayari kuitumikia muda wowote watakaihitaji huduma yake.

Deniss ambaye ni ndugu na Moses Odhiambo aliyewahi kuichezea Yanga miaka ya nyuma  amevutiwa sana na namna Yanga ilivyocheza kwenye mechi iliyopigwa Jumatano ( September 3 ) kwenye dimba la uwanja wa taifa ambapo timu yake ya Thika ililala bao 1-0.

“ Nimevutiwa sana na soka ya Yanga, ki ukweli wanacheza vizuri sana, nipo tayari kuipokea ofa yeyote kutoka kwao” alisema Kiungo huyo aliyengara katika mchezo huo wa Jumatano.