Breaking News
Loading...
Monday, 2 March 2015

Info Post


Marehemu Adamu ni moja kati ya makocha waliopata kunifundisha soka kwa kipindi kirefu ,katika moja ya hadithi zake nyingi alizokuwa akitusimulia yeye na Mzee Kilambo  aliwahi kutusimulia mechi iliyopigwa miaka ya sabini mwishoni dhidi ya timu yake ya Simba Sports Club na TPC ya Moshi,mechi ambayo iliishia kwa Simba kushinda goli mbili  kwa bila na yeye Adam  Sabu maarufu kama Gud mullar alitupia yote mawili.
Sabu alituambia wakati ule Simba ilikuwa imemsajili kijana mmoja ambaye alikulia Morogoro wakati Sabu anacheza mpira karikuwa katoto kadogo mno,sasa ndio roho ya Simba chochote atakachosema viongozi watakuwa wanamsikiliza yeye,alikuwa anaitwa Aluu Ally,kwa wale waliopata bahati ya kumuona watakubaliana nami kuwa Aluu Ally ni moja kati ya viungo bora kabisa waliopata kutokea katika Nchi yetu.
Wakati mchezo umemalizika Sabu akitoka na furaha ya kufunga magoli mawili Aluu Ally alitoka analia ,hakupenda kabisa matokeo yale na  viongozi wa Simba walipomfuata kumnyamazisha na kumuuliza kulikoni alijibu Simba ni timu kubwa huwezi kuwa na wachezaji wa aina ya Adam Sabu nimempa mipira 18 pasi za uhakika anafunga goli mbiliii!!!! Hafai kuwepo katika timukubwa  kama hii, Sabu alilia saana baada ya kusikia kauli hiyo ya kijana huyo aliyemwacha Morogoro akiwa Kinda kabisa ndio soka lilivyo.
Haraka sana nikamkumbuka Said Bahanuzi aliyepelekwa kwa mkopo Polisi ,nimeshuhudia mechi zake karibu tatu alizocheza akiwa na Polisi moja ikiwa pale Mkwakwani alikosa magoli mengi mno, mechi nyingine ni ya juzi tu tuliyoiona kupitia Azam Tv dhidi ya Kagera Sugar pale Kambarage Shinyanga ambapo walifungwa goli moja kwa bila nay eye  Bahanuzi akiwa amepoteza baadhi ya nafasi za wazi mno ,niliwauliza viongozi wake baada ya mchezo kwisha  wakaniambia leo bhana afadhali Mtwara dhidi ya Ndanda alikosa karibu Kumi za wazi,vijana akina Bantu Admin,Mgangai kazi yao wenyewe ni kumpelekea tu Bahanuzi ashindwe na timu haina mashabiki akikosa wanarudi kati kukaba.
Ni lazima nikiri kuwa miongoni mwa watu walioshiriki kumpeleka Yanga kwa njia moja au nyingine alikuwa ni mwandishi wa makala hii na kweli aliingia na kufanya vizuri mno katika michuano ya Kagame na kuibuka kuwa mfungaji bora,basin a soka lake akaliacha katika michuano hiyo,kukawa na hadithi nyingi zinazomuhusu yeye za nje ya uwanja,Maskini Bahanuzi hakupata mtu wa Saikoloji jiji akaliingia kwa pupa soka likamshinda,pamoja na kuitwa timu ya Taifa bado kocha aliona bado anahitaji marekebisho makubwa kwake ili awe mchezaji wa timu kubwa.
Wiki iliyopita nilistushwa kusikia Said Bahanuzi amekuwa mchezaji bora wa mwezi,naweheshimu wataalamu hao wanaochagua wachezaji bora wa mechi lakini sikuelewa kama kweli wana vigezo gani muhimu kumpitisha mchezaji huyo ambaye kwangu me naona amewanyima nafasi nyingi mno Polisi za kuibuka na ushindi na naamini hata kama angeulizwa Kocha Adolf Richard asingemtaja Bahanuzi.
Bahanuzi soka lake sasa limehamia mdomoni kila kukicha anaeleza habari za kishirikina tu na anasahau soka na mambo hayo ni kiini macho tu na ninavyomfahamu Said ni mtu wa Ibada mno ni vipi aweke imani kubwa mno katika mambo ya giza, ndio maana Mbwana Samata,Thomas Ulimwengu wasoka nje ya nchi kwa juhudi za mazoezi tu,ni kawaida ya wachezaji wengi mno wanaofikia umri mkubwa wanaanza kuongea na mpira unahamia mdomoni zaidi kuliko kwenye miguu.
Kwa Bahanuzi umri wake bado ni mdogo hivyo ana kila sababu ya kusahau mambo ya timu kubwa kama Simba na Yanga zenye washabiki wengi wenye uwezo mkubwa wa kusoma timu zao na hawakosekani katika viwanja ,lakini mbaya zaidi hawana subira na mtu wa aina ya Bahanuzi anayepata nafasi 18 na kufunga goli moja hapo ndipo nilipomkumbuka kocha wangu Adamu Sabu.
Bahanuzi acha kuongea piga soka watu wataona lakini kwa kiwango chako cha sasa mmmm bado me Napata shaka maana soka linachezwa uwanjani sio chumbani wote tunaliona,na tayari umetoa masharti yanga wakitaka urudi wakuhakikishie nafasi ya kucheza kwa maana hiyo ,Msuva,Nyonzima ,Tambwe,Ngasa na Contihon watupwe nje uwepo ndio hapo nachoka kabisaa
Mwandishi wa makala hii anapatikana Email kennedymwaisabula@gmail.com