Breaking News
Loading...
Tuesday, 3 March 2015

Info Post
Shirikisho la soka Tanzania (TFF) limeangusha adhabu kwa

baadhi ya timu za Ligi Daraja la Pili baada ya kubaini uvunjaji

wa kanuni uliofanywa na timu hizo.
Tarrifa iliyotolewa jijini leo kupitia kwa msemaji wa TFF

Baraka Kizuguto baadhi ya timu zilizopata adhabu ni Ujenzi

Rukwa na Volcano FC ya Morogoro huku pia baadhi ya

viongozi na wachezaji nao wakiadhibiwa.
Ujezi Rukwa na Volcano zimeshushwa daraja mpaka ligi ya

Wilaya baada ya kushindwa kufika uwanjani kwenye mechi

zao dhidi ya Mvuvumwa na Wenda, Magereza Iringa imetozwa

faini ya Tsh. 200000 baada ya kuchelewa kwenye kikao cha

maandalizi ya mechi, AFC imetozwa Tsh. 300000 baada ya

mashabiki wake kufanya vurugu kwenye mechi dhidi ya

Bulyanhulu wakati viongozi wa Mbao FC Abdallah Chuma

na Yasin Abdul wakifungiwa miezi sita na Faini ya Tsh.

100000 kila mmoja baada ya kumtukana nakumtishia maisha

Kamishina wa mechi dhidi ya AFC
Singida United imepewa pointi tatu dhidi ya Ujenzi Rukwa ambayo ilimchezesha mchezaji asiyestahili.