Breaking News
Loading...
Thursday, 5 March 2015

Info Post


.
Miezi miwili iliyopita nilitembelea mitaa ya Kigamboni nikakutana mzee moja mshabiki mkubwa sana wa ile iliyokuwa Sunderland yaani sasa ni Simba anaitwa Nassoro Mkutuka mtunzi wa mashairi maarufu kwa jina la Hailati,aliniambia bwa mdogo nenda kaandike makala Kaseja hawezi kurudi Simba aslani,sikuamini akanisisitizia kuwa kamwe hatotokea mchezaji kucheza Simba zaidi ya miaka kumi,nikabaki nimeduwaaa,nikavuta hisia na kuamua kuandika makala hii.

Zamoyoni Mogela ' Golden Boy' alianza kuchezea Simba akitokea timu ya Taifa mwaka 1982 ,Juma Kaseja alianza kuchezea Simba 2003  baada ya kusajiliwa 2002,wenye Simba wenyewe wanasema kamwe mchezaji wao hawezi kucheza zaidi ya miaka 10 na ndivyo ilivyokuwa kwa kina Adamu Sabu,Abdalh Kibaden  Mohamedy Mwameja aliyesajiliwa mwaka 1992 na wengineo.
Mogela ambaye alisajiliwa na wenzake akina Malota Soma na Sospeter Mwaluko alikuwa kipenzi mno cha mashabiki na wanachama wa Simba Sports club,aliondoka Simba kwa tuhuma nzito toka kwa viongozi wa wakati ule akina  Juma Salum na kuwafanya mashabiki kuamini na kumfanya Mogan kupoteza marafiki wake wengi waliokuwa wakimuhusudu kupita kiasi.

Akisimulia kwa kinywa chake Mogan ambaye wakati alizushiwa balaa  kwa kuwa alikuwa ni kiongozi wa wachezaji  yaani Kapten na muda wote alikuwa ni mtetezi wa wachezaji wenzake jambo ambalo viongozi huwa hawalitaki na hawalipendi kabisa.
Uongozi wa wakati huo ambao ulikuwa ukiongozwa na Mzee Juma Salum na wafadhili wao wakuu kabisa akina Azim Dewj na Ahmedy Bora walimtuhumu Zamoyoni Mogela kuwa mara zote huwa hawafungi Yanga kwa kuwa tu anahongwa na Abass Gulamali ambaye alikuwa ni mfadhili mkuu wa timu hiyo,kitendo kilichomuuma sana mkongwe  huyo ambaye kwake Simba ilikuwa ni sehemu ya familia alicheza kwa moyo woteee.Capten zamoyoni Mogela akaliacha jahazi mwishoni mwa mwaka 1991 akapumzika nyumbani kwa muda wa Mwaka ndipo upande wa upinzani ukiongozwa na  Waziri wa Fedha wakati ule akishirikia kwa karibu na mfadhili wao Abass Gulamali na Majid Seif wakannyakua mtaalamu.
Naiangalia njia hiyo ya Mogan naiona ndio ya Juma Kaseja leo, akiwa ni kiongozi wa wachezaji kama ilivyokuwa kwa Zamoyoni Mogela naye pia ni mtetezi wa wenzake jahazi kaliachia , ametua Yanga Afrikani na kuungana na makipa wenzake aliowahi kucheza nao Simba Ally Mustafa Barthez na Deogratus Munish Dida ,ametumikia timu ya Simba kwa mapenzi makubwa mnoo na amekuwa na marafiki wengi ndani ya timu leo anawaacha kwa sababu tu ya viongozi kumwekea maneno yasiyo yake kama alivyowekewa Zamoyoni Mogela miaka ile, au ndio kile kivuli cha wazee wale wa Sunderland ,kama ni hivyo inasikitisha mno.

Alichokifanya  Marehemu Abbas Gulamali miaka ile ndicho alichokifanya Manji leo akiwatumia majemedari wake Seif Magari na Abdalah Bin Kleb sina hakika na yule aliyekuwa Waziri wa Fedha wakati ule kama na hili kashiriki maana naona kwa sasa ana majukumu makubwa mno ya Kitaifa.
wengi tulikuwa tunajiuliza nini kinachowasukuma mashabiki kuruhusu nyota wao waliodumu katika timu kipindi kirefu lakini iwe mwisho miaka tu,ninini kimefichwa na wazee wale akina Mkutuka ambacho sisi vijana wa leo hatukijui!!!.
Basi kama ndio hivyo nenda Kaseja usipinge kauli za wazee hata kama timu unaipenda vipi,hata kama bado una uwezo wa kiasi gani hapana wazee waliotangulia wanasema Simba mwisho miaka  kumi tu ime nimebaki nimeduwaa na kuwaachia wapenzi wasomaji kufanya utafiti wa kina katika suala .