Breaking News
Loading...
Thursday, 5 March 2015

Info Post


Katika moja kati ya  hotuba zake Baba wa Taifa mwalimu Julias Kambarage Nyerere aliwahi kuizungumzia Afrika na kuisikitikia mno Afrika ,anasema alikuwa hajui kama Afrika  ni tegemezi tegemezi tegemezi kweliiii,tegemezi ki uchumi ,kisiasa na kila kitu,Afrika kila kitu inategemea kwa Wazungu na mbaya zaidi hata mawazo yao yanatoka kwa Wazungu alisema ni tegemezi tegemezi tegemezi saaana,aliwaona wale Mazungu Karne ijayo yatakuwa mbali mno na sisi ,na sisi  tutaendelea kuwa kama Madodoki ni kupokea tu iwe uchafu au usafi,alifika mbali ,mno na kusema kuwa Afrika itakuwa kama Mbuga kubwa mno wazungu watakuwa wanakuja kama watalii tu kwetu.
Wiki iliyopita timu ya Stand United ilimtimua kocha wake Emanuel Masawe kwa kile uongozi walichodai kuwa anawagawa wachezaji, na kuwa ndio chanzo cha timu hiyo kufanya vibaya,kwangu mimi sikushangaa na kauli hiyo kwani ni ya kawaida mno kwa viongozi wetu wa soka punde wanapowatimua makocha wao.
Kilichonivutia zaidi kwa kocha Masawe ni siku moja baadaye kufunguka na kusema kile kilichomuondoa na ambacho makocha wengi simaanishi wazalendo ni wale wanaofundisha soka  Tanzania bila kujali wametoka Zambia ,Serbia au kwingineko wamekuwa tegemezi tegemzi tegemezi kweli katika hilo,Masawe alikataa kupangiwa list na viongozi na mbaya zaidi hata mazoezini hawaonekani,safi sana Kocha Masawe safi mnoooo.
Makocha wengi wanaofundisha soka Tanzania wanawaogopa viongozi wanaowalipa vi mishahara vya kawaida mno kwa kuwa tu hawana shughuri nyingine yeyote ya kuwaongezea kipato zaidi ya soka leo wamejikuta wakiwa tegemezi kwa kila kitu kuanzia kufundisha hadi kupanga timu wamekosa kabisa meno kulingana na taaluma yao,Masawe leo kanikumbusha jinsi makocha tunavyotakiwa tuwe ni vyema asubuhi tukauza Nyanya jioni tukaenda kufundisha Mpira.
Takriban miaka minne iliyopita nilikuwa katika kipindi kimoja cha TV na wadau wengi wa soka ,baadhi ya waliokuwepo kwa sasa ni viongozi wakubwa kabisa ndani ya club ya Simba(Kaburu,Tully),viongozi wale ambao kwa wakati ule mmoja alikuwa simba na mwingine Ashant ,mmojawapo alisema Tanzania hakuna Makocha ,sisi kocha wetu Patrick Phill tunampangia sisi list ya kucheza,nilisimama kuipinga mno hoja hiyo kama kocha na bahati mbaya nimefundisha timu nyingi za mjini Dar kuanzia Ashant,Villa Squad,Vijana Ilala,Moro United,Yanga Afrikan,Bandari Dar na Mtwara kasoro simbakote huko kama kuna kiongozi aliyesubutu kuniingilia kwenye list nadhani alikutana na makali yangu ,Muhsin Baraboo pale vijana,Msafiri Mgoyo pale Ashant,Kifukwe na Malinzi pale Yanga,Godigodi pale Villa na Ismail Aden Rage pale Moro hao wote wananitambua sikuwahi kuwa tegemezi kwa kuwa mimi nauza kwanza nyanya soka baadaye.
Makocha ambao tulidhani ndio ngozi nyeupe au wanatoka nje  labda wataheshimu taaluma yao ndio hao wanapangiwa list,leo timu inacheza Zanzibar katika maandalizi yote ya kombe la mapinduzi mchezaji hayupo ,yupo kwao tena mapumzikoni anarudi kocha Mzungu anampanga kesho kama hajapangwa na viongozi atakuwa amepangwa na nani!!!!!! Safi sana masawe.
Wapo makocha wamekuwa na misimamo hadi unasikia raha ndugu yangu Sebastian Nkoma ni kocha maskini kabisa lakini kila siku misimamo yake inamfanya viongozi wamwone hafai na yeye kwa ku heshimu taaluma anamwaga vumbi,Eugen Mwasamaki pamoja na umaskini akiwa timu ya Tesema leo inamilikiwa na Halmashauri ya Kinondoni  hakukubali kuyumbishwa na watu wanaojiita wa mpira wakati ni madiwani tu na wengine hawajui kabisa mpira zaidi za kuwa Wahasibu tu wa Halmashauri ,alipoambiwa aondoke saa 3 asubuhi yeye saa 12 alfajiri alikuwa tayari kafungasha virago karudi Karume kufundisha timu za watoto bureeee kabisaa,Mbeya City tumeshuhudia kocha  Juma Mwambusi  akiwaumbua mashabiki na viongozi wake kuwa maisha yake yote ataheshimu taaluma akabwaga manyanga wenyewe wakamrudisha ,Tanzania tumebaki na makocha wachache mno wa aina hiyo wengi wamekuwa ni mizigo ,na akili zao zimeshikiwa na viongozi na mbaya zaidi viongozi hao ndio wanaopita kwa mashabiki na kuwaambia kesho tutamwambia mwalimu apange list ya wazawa watupu hao wageni tupa nje na kweli kesho unakuta listi ya wazawa watupu mbele unamwona Javu unamwona Tegete ndio makocha wetu.
Makocha wanaofundisha Tanzania bila kujali wanatoka nchi gani ,kama atakaa zaidi ya miezi sita nchini huyo sio kocha lazima atapangiwa listi,Trot Moloto moja kati ya makocha bora Afrika kusini alipoambiwa neno moja tu panga list hii yeye aligongo viza yake kurudi kwao na hajaonekana tena huyo ndio mfano wa kocha.
Makocha mnaofundisha soka Tanzania mtaendelea kuwa tegemezi tegemezi hadi lini,ukocha ni taaluma ingawa kila mtu anajifanya anajua ukocha ndio maana leo nawapa bravo Juma Mwambusi mbeya city na Emanuel Masawe Stand United.
Mwandishi wa makala hii ni mfanyakazi wa Mamlaka ya usimamizi Bandari anapatina Kennedymwaisabula@gmail.com 06528757YANGA MALIZENI MECHI TAIFA NA SI VINGEVYO.
Mwaka 1973 nikiwa darasa la kwanza Simba Sports Club ikiwa ndani ya uwanja wa Taifa katika mechi yake ya Club Bingwa ya Afrika ngazi ya nusu fainal ilikutana  na  timu toka Misri inaitwa Mehal El Cubra ,hadi mwisho wa mpambano huo ambao sisi tuliokuwa watoto tulikuwa tuna njia nyingi mno za kuingia uwanjani sijui siku hizi watoto wa leo wana njia zipi ,lakini sisi tulikuwa tunaweza kuwahi kufunga nyavu na kupachika Vibendera,kuruka ukuta ambao kwa wakati ule ulikuwa ni mrefu sana kulingana na vimo vyetu lakini tutafanyaje,au nimshike mkono mtu yeyote mzima niingie naye,achilia ile ya kukaa juu ya miti na kusubiri dakika 10 za mwisho fungulia Mbwa,Simba ilikuwa imeibuka na ushindi wa goli moja kwa bila goli lililofungwa na Saady Ally nalikukmbuka hadi leo miaka zaidi ya 40 imepita.
Watanzania wengi walijua kuwa kuwa Simba imemamaliza mchezo tayari na ukizingatia mziki uliokuwepo wakati ule ukiongozwa na Athuman Mambosasa golini wengine Shaban Baraza,Mohamedy Kajole,Omary Chogo,Haidar Abeid,Halid Abeid ,Willy Mwaijibe,Adam Sabu ,Abdalh Kibadeni, na wengineo wengi tu ni kwa nini tufungwe!!!!!! Kumbe wapi tukaonewa tukapigwa tukazomewa na mwisho wa siku tulipigwa goli moja na katika eneo la penalt tano tano Marehemu Mambosasa angekuwepo angesimulia tukayaaga mashindano fainal tukaikosa hatukujua mbinu za kumaliza mchezo.
Mwaka 1985 nikiwa nacheza timu ya soka ya Mwadui tulipata bahati ya timu nzima kwenda na gari letu mjini Mwanza chini ya kiongozi wetu Chief Kihiyo kwenda kushuhudia pambano la club bingwa ya Afrika kati Simba na National El Ahaly  ya Misri,niliishuhudia timu hiyo ya Misri ikitumia dakika 10 tukamaliza mchezo baada ya kupiga basi karibia 30 hivi na kumpelekea mfungaji wao bora kabisa wakati huo tena Barani Afrika Mohamud El Hatibu maarufu kama Bibo ambaye alimshambua kiraini kabisa kipa Mozes Mkandawile,ingawa matokeo ya mechi ile hadi mwisho Simba iliibuka na ushindi wa magoli 2-1 magoli yaliyofungwa na Zamoyoni Mogela na Mtemi Ramadhani lakini  wa Misri  wale walishamaliza mchezo dakika 10 tu za mwanzo wenzetu wanaojua soka ndicho kitu walichotuzidi kujua kumaliza mchezo.
Mnamo miaka ya 80 katikati Yanga walikumbana tena na timu toka Misri na mechi ya awali walianza Misri ,yanga ikijengwa na ukuta wa Berlin uliongozwa na Athuman Juma Chama,Yusuph Bana,Ahmedy Amasha ,Allan Shomari wenyewe wakimwita Moringe,Juma Mkambi ,Fred Minziro golini akiwa Juma Mhina ,pamoja na ugumu wa ukuta huo iliwachukua dakika 10 za mwisho baada ya kumchosha mno Amasha na kuandika goli 5 na baada ya dakika 90 ubao ulisomeka 5-1 mechi wakawa wameshaimaliza hapa wakaja kutalii tu na kutoka sare 1-1 na bahati kocha msaidizi wa Yanga leo Charles Boniface Mkwasa alikuwepo katika mechi hiyo na goli moja alifunga yeye.
Yanga  wiki hii inakumbana na timu kutoka Zimbabwe inaitwa Platinum ni lazima imalize mchezo Dar es saalam na si sehemu nyingine yeyote,wawakilishi wenzao Azam Walishindwa kumaliza mchezo pale Chamazi matokeo yake ndio hayo tuliyoyasikia,ili umalize mchezo ni lazima kila nafasi inayopatikana watu washangilie  bao,ni lazima tuwe na hazina kubwa ya mabao nyumbani,kwa wenzetu wanaojua kumaliza mchezo watakuja wakiwa wameficha makucha yao huenda hata washambuliaji wao muhumu kama vile sisi  Msuva na Ngasa huenda wakakaa jukwaani wanatusoma tu ili waje wamalize mchezo kwao.
Kocha Mdachi Hans Pluijm na bench lake la ufundi  ni lazima wafundishe wachezaji faida ya kutumia kila nafasi wanayoipata kwa kuweka mpira kambani kinyume cha hapo tutatafuta sababu nyingi mno katika mechi ya marudiano pale Harare wiki mbili baadaye,ni lazima timu iwe na hazina ya magoli yasiyopungua manne kinyume na hapo mchezo tutakuwa hatujaumaliza dar na mchezo unatakiwa umalizwe katika uwanja mkuu wa Taifa siku ya terehe 14 March.
Timu nyingi za kwetu kuanzia wachezaji ,viongozi na mashabiki hatujui sehemu ya kumalizia mashindano ndio maana usiku ule katika uwanja wa Chamazi kwenye mechi ya Azam na El Merreck ya Sudan wakati wachezaji ,viongozi na mashabiki wakati wakishangilia ushindi ule wa magoli mawili wenye kuangalia kwa jicho la tatu muda huo huo tukasema mchezo huu bado haujaisha utakwenda kwisha Sudan,Yanga tunatakiwa tuwe na mshikamano mkubwa ushindi wowote wa goli chache tujue mchezo haujaisha!!!!!
kennedymwaisabula@gmail.com