Breaking News
Loading...
Monday, 9 March 2015

Info Post


Kuzidiwa katika safu ya kiungo sambamba na benchi la ufundi kushindwa kusoma mchezo kwa umakini, vimetajwa kuwa sababu kubwa iliyopelekea Yanga kukubali kichapo cha bao 1-0 jana mbele ya Simba.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na mwandishi wetu, baadhi ya makocha wa soka nchini wamesema kuwa safu ya kiungo ya Yanga ilishindwa kuwamudu viungo wa Simba ambao walitawala vilivyo kwenye mechi hiyo.
“Pluijm alianza na viungo wawili wakati Simba walikuwa na viungo wengi ambao wanajua kumiliki mpira. Pia benchi la ufundi la Yanga nadahni lilishindwa kusoma na kuuelewa kwa haraka mchezo, “ alisema Eugene Mwasamaki.
Nae Kocha Msaidizi wa Stand United Athumani Bilali, alisema kuwa Simba walicheza kitimu hasa safu yao ya kiungo wakati Yanga waliingia wakitegemea uwezo wa mchezaji mmoja mmoja.
Ushindi dhidi ya Yanga umewapeleka Simba mpaka nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi wakiwa na 26 huku Yanga wakiendelea kuongoza wakiwa na pointi 31
Wachezaji wa Simba wakishangilia bao la Okwi