Breaking News
Loading...
Monday, 9 March 2015

Info Post


Mshambuliaji wa Kagera Sugar Rashid Mandawa amesema kuwa ataendelea kula sahani moja na Mrundi Didier Kavumbagu katika kuwania zawadi ya mfungaji bora wa Ligi Kuu msimu huu.
Mandawa aliye kwenye kiwango cha juu hivi sasa, ameshafunga mabao nane wakati Kavumbagu anayeongoza ameshatumbukiza nyavuni mabao tisa jambo linalozidi kuleta ushindani baina yao.
Akizungumza na Mwandishi wetu jana, Mandawa alisema lengo lake ni kuibuka mfungaji bora wa ligi kuu na pia kuisaidia Kagera Sugar imalize ikiwa katika nafasi nzuri kwenye msimamo wa ligi hiyo.
“Kavumbagu ni mshambuliaji mzuri anayezidi kunihamasisha mimi kufanya vizuri. Nataka nilipe fadhila kwa timu yangu ya Kagera ninataka imalize ligi ikiwa kwenye nafasi za juu,” alisema Mandawa
Mandawa ni miongoni mwa washambuliaji wazawa ambao wamekuwa kwenye kiwango cha juu kwa kuzifumania nyavu na kuleta ushindani kwa wageni ambao walikuwa wakitawala.