Breaking News
Loading...
Friday, 6 March 2015

Info Post
Mwamuzi wa kati Israel Nkong'o kutoka hapa nchini,

anatarajiwa kushika kipyenga kwenye mechi ya kombe la Ligi

ya Mabingwa Afrika kati ya Zesco United ya Zambia  na

AS Kaloum ya Guinea utakaofanyika Machi 13 huko nchini

Zambia.
Nkong'o atakuwa akisaidiwa na  Watanzania wenzake John

Kanyenye na Josephat Bilali huku mezani akiwepo Waziri

Sheha wakati Kamisaa wa mchezo huo akiwa ni Elvin Mshani

kutoka Afrika Kusini.
Wakati huohuo Shirikisho la Soka Tanzania (TFF),

limetangaza viingilio kwa ajili ya mechi ya Yanga na Simba

utakaochezwa Jumapili hii jijini.
Jukwaa la VIP A bei ya tiketi ni shilingi 40,000, VIP B silingi

30,000, VIP C  elfu 20, 000 wakati viti vya rangi ya kijani na

bluu bei ya tiketi itakuwa ni shilingi elfu saba.
Kizuguto pia alitaja vituo vitakavyotumika kuuzia tiketi kuwa ni

Oil Com Buguruni, Big Bon Kariakoo, Stendi ya daladala

Makumbusho, TFF Karume, Dar Live Mbagala na

Mgahawa wa Steers Posta mpya.
TFF imewataka mashabiki wa soka watakaojitokeza uwanjani

siku hiyo kutoingia na chupa za maji, mabegi au silaha uwanjani

hapo kwani ulinzi utakuwa ni wa uhakika huku pia idadi ya

magari yatakayoingia uwanjani siku hiyo yakitakiwa kutozidi

mia.