Breaking News
Loading...
Thursday, 9 April 2015

Info Post
Beki wa kati Matts Hummels anayechezea Borussia

Dortmund, amesema kuwa ataamua hatma yake ndani ya

klabu hiyo ndani ya kipindi cha wiki chache zijazo.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26, mkataba wake ndani

ya timu hiyo ya Dortmund umebakiza kipindi cha miaka miwili

lakini kumekuwa na hofu ya mlinzi huyo wa Kimataifa wa

Ujerumani kutimka mwishoni mwa msimu huu ikiwa timu hiyo

haitafanikiwa kupata nafasi ya kucheza Ligi ya Mabingwa

msimu ujao.
Inadaiwa kuwa Manchester United ni miongoni mwa timu

ambazo zimekuwa zikiisaka kwa udi na uvumba saini ya

Hummers, ikitajwa kuwa wametenga kiasi cha Pauni milioni 35

ili kumnasa beki huyo.
Hata hivyo Hummers amekanusha kuwa anaangalia kama

Dortmund itaingia kwenye Ligi ya Mabingwa kama wengi

wanavyovumisha na amepanga kupeleka maoni yake kwa

uongozi wa timu hiyo juu ya usajili kwa ajili ya msimu ujao.
"Siwezi kukubaliana na hali kama hiyo kwa namna moja au

nyingine. Ninaongozwa na akili yangu kufanya maamuzi.

Mambo yatakuwa wazi baada ya wiki chache," alisema

Hummers.
Kauli ya Hummers huenda ikaongeza presha kwa Dortmund

ambayo ipo kwenye nafasi ya kumi katika msimamo wa Ligi

Kuu nchini Ujerumani maarufu kama 'Bundesliga'